Bahari za
Ushairi
Bahari za ushairi ni nyingi sana. Shairi huainishwa katika
bahari fulani kulingana na mtindo wake, umbo lake na matumizi ya lugha.
Baadhi ya bahari za ushairi ni:
- Utenzi - shairi ndefu lenye kipande kimoja katika kila mshororo.
- Mathnawi - ni shairi la vipande viwili (ukwapi na utao) katika kila mshororo.
Ewe mtunga silabi, na sauti ya
kinubi,
Majukumu hatubebi, maadamu hatushibi,
Mateso kwa ajinabi, kwa mabwana na mabibi
Ukija hayatukabi, karibia karibia
Majukumu hatubebi, maadamu hatushibi,
Mateso kwa ajinabi, kwa mabwana na mabibi
Ukija hayatukabi, karibia karibia
- Ukawafi - ni shairi la vipande vitatu (ukwapi, utao na mwandamo) katika kila mshororo.
Nashindwa nikupe nini, nishukuru kwa
malezi, mapenzi na riziki,
Ni pendo kiasi gani, lishindalo la mzazi, kweli mama hulipiki,
Ulinilinda tumboni, ukilemewa na kazi, ila moyo huvunjiki,
Kanilisha utotoni, mavazi pia malazi, ukitafuta kwa dhiki.
Ni pendo kiasi gani, lishindalo la mzazi, kweli mama hulipiki,
Ulinilinda tumboni, ukilemewa na kazi, ila moyo huvunjiki,
Kanilisha utotoni, mavazi pia malazi, ukitafuta kwa dhiki.
- Mavue - Shairi la vipande vinne (ukwapi, utao, mwandamo na ukingo) katika kila mshororo.
Sisi walipa ushuru, wajenga taifa,
tena kwa bidii, twahangaishwa,
Tumenyimwa uhuru, tuna mbaya sifa, hatujivunii, tunapopotoshwa,
Kila tunapopazuru, damu na maafa, hatutulii, hali ya kutishwa
Tumenyimwa uhuru, tuna mbaya sifa, hatujivunii, tunapopotoshwa,
Kila tunapopazuru, damu na maafa, hatutulii, hali ya kutishwa
- Ukaraguni - shairi ambalo vina vyake vya kati na vya mwisho hubadilika kutoka ubetio mmoja hadi mwingine.
Vina Ubeti 1: ---ni, ---mi,
ubeti 2: ---ta, ---lo,
ubeti 3: ---po, ---wa,
ubeti 2: ---ta, ---lo,
ubeti 3: ---po, ---wa,
- Ukara - shairi ambalo vina vya kipande kimoja havibadiliki kutoka ubeti mmoja hadi mwingine, lakini vina vya kipande kingine hubadilika. Kwa mfano, vina vya kati vinafanana kutoka ubeti wa kwanza hadi wa mwisho lakini vina vya kipande cha mwisho vinabadilika kutoka ubeti mmoja hadi mwingine.
vina Ubeti 1: ---shi, ---ma,
ubeti 2: ---shi, ---ko,
ubeti 3: ---shi, ---le,
ubeti 4: ---shi, ---pa
ubeti 2: ---shi, ---ko,
ubeti 3: ---shi, ---le,
ubeti 4: ---shi, ---pa
- Mtiririko - shairi ambalo vina vyake vya mwisho na vya kati havibadiliki kutoka ubeti wa kwanza hadi wa mwisho.
kwa mfano vina vikiwa ( ---ni,
---ka) kutoka ubeti wa kwanza hadi wa mwisho.
- Mkufu/pindu - Shairi ambalo neno la mwisho au kifungu cha mwisho cha maneno katika ubeti mmoja, hutangulia katika ubeti unaofuatia.
Hakika tumeteleza, na njia
tumepoteza,
Nani wa kutuongoza, aliyepewa uweza,
Filimbi akipuliza, tusiyeweza kupuuza,
Bali twaisikiliza, bila ya kuzungumza,
Bila ya kuzungumza, wala mwendo kulegeza,
Tumwandame ja mwangaza, kututoa palipo giza,
Penye dhiki ya kuliza, bila sauti kupaza
Pengo hili kulijaza, ni nani anayeweza,
Nani wa kutuongoza, aliyepewa uweza,
Filimbi akipuliza, tusiyeweza kupuuza,
Bali twaisikiliza, bila ya kuzungumza,
Bila ya kuzungumza, wala mwendo kulegeza,
Tumwandame ja mwangaza, kututoa palipo giza,
Penye dhiki ya kuliza, bila sauti kupaza
Pengo hili kulijaza, ni nani anayeweza,
- Kikwamba - Neno moja au kifungu cha maneno hurudiwarudiwa kutanguliza mishororo au ubeti katika shairi.
Jiwe hili lala nini, ila moshi na
majani,
Jiwe linalala lini, litokapo vileoni,
Jiwe hili halineni, lina macho halioni,
Jiwe na tulibebeni, tulitupe mitaroni
Jiwe linalala lini, litokapo vileoni,
Jiwe hili halineni, lina macho halioni,
Jiwe na tulibebeni, tulitupe mitaroni
- Kikai - Shairi lenye kipande kimoja kifupi (chenye mizani chache kuliko kingine) Mfano (8,4)
Nani binadamu yule, adumuye,
Anayeishi milele, maishaye
Jenezani asilale, aluliye,
Kaburi liko mbele, sikimbiye.
Anayeishi milele, maishaye
Jenezani asilale, aluliye,
Kaburi liko mbele, sikimbiye.
- Msuko - Shairi ambalo kibwagizo/mshororo wa mwisho ni mfupi kuliko mishororo mingineyo. K.v (8,8) (8,8) (8,8) (8).
Hawajazawa warembo, usidhani
umefika,
Ukisifiwa mapambo, jinsi ulivyoumbika,
Akipata jipya umbo, 'tabaki kihangaika,
Usidhani umefika.
Ukisifiwa mapambo, jinsi ulivyoumbika,
Akipata jipya umbo, 'tabaki kihangaika,
Usidhani umefika.
- Mandhuma - shairi ambalo kipande kimoja hutoa hoja, wazo ama swali, huku cha pili kikitoa jibu/suluhisho.
- Malumbano - Mashairi mawili ambapo mshairi mmoja hutunga shairi akijibu au kupinga utunzi wa mshairi mwengine.
- Ngonjera - Shairi lenye wahusika wawili wanaojibizana. K.m. Ubeti wa kwanza, mwalimu, na wa pili, mwanafunzi.
- Sakarani - Shairi lenye bahari zaidi ya moja.
- Sabilia - Shairi lisilokuwa na kibwagizo. Kituo (mshororo wa mwisho) hubadilika kutoka ubeti hadi ubeti.
- Shairi huru - shairi lisilozingatia sheria za ushairi
- Shairi guni - shairi lenye makosa ya arudhi za shairii
19.
Aina za Mashairi
20.
Zifuatazo
ni aina za mashairi kulingana na idadi ya mishororo katika kila ubeti
AINA
|
#MISHORORO
|
MFANO
|
Umoja/tathmina
|
1
|
|
Tathnia
|
2
|
|
Tathlitha
|
3
|
|
Tarbia
|
4
|
|
Takhmisa
|
5
|
|
Tasdisa
|
6
|
|
Usaba
|
7
|
|
Ukumi
|
10
|
21.
Tanbihi: Aina za Mashairi ni tofauti na Bahari za Ushairi. Aina za
mashairi huzingatia idadi ya mishororo katika kila ubeti ilhali Bahari za
Shairi hutegemea na muundo wa shairi kwa kuzingatia vina, mizani, vipande na
mpangilio wa maneno. Shairi moja haliwezi kuwa la aina mbili (k.v tarbia na
takhmisa) lakini shairi linaweza kuwa katika bahari zaidi ya moja.
Istilahi za Kishairi
Haya ni baadhi ya maneno ambayo hautakosa kukutana nayo
unapozingatia ushairi. Ni muhimu mwanafunzi kuyajua vizuri.
- Shairi - ni sanaa ya maneno (utunzi maalum wa lugha ya kisanaa) unaotumia mpangilio na uteuzi maalum wa maneno na sauti ili kupitisha ujumbe fulani.
- Vina - ni silabi za mwisho katika kila kipande.
- Mizani - ni idadi ya silabi katika kila mshororo.
- Mshororo - ni msitari mmoja wa maneno katika shairi.
- Ubeti - ni kifungu cha mishororo kadhaa.
- Vipande - ni visehemu vya mshororo vilivyogawanywa kwa alama ya kituo(,)
- Ukwapi - kipande cha kwanza katika mshororo
- Mwandamo - Kipande cha tatu katika mshororo
- Ukingo - kipande cha nne katika mshororo
- Utao - kipande cha pili katika mshororo
- Mwanzo - mshororo wa kwanza katika ubeti
- Mloto - mshororo wa pili katika ubeti
- Kimalizio/Kiishio - mshororo wa mwisho katika ubeti usiorudiwarudiwa katika kila ubeti.
- Kibwagizo - mshororo wa mwisho katika ubeti unaorudiwarudiwa kila ubeti.
Sifa za Ushairi
- Huwa na vina, mizani, mishororo na beti
- Hutumia lugha teule
- Hufupisha au kurefusha maneno ili kutosheleza idadi ya mizani
- Mashairi hayazingatii kanuni za kisarufi. (Angalia uhuru wa mshairi)
- Hutumia mbinu za lugha
Umuhimu wa Mashairi
- Kuburudisha
- Kuhamasisha jamii
- Kukuza sanaa na ukwasi wa lugha
- Kuliwaza
- Kuelimisha
- Kuonya, kutahadharisha, kunasihi na kuelekeza
- Kupitisha ujumbe fulani
- Kusifia mtu au kitu
- Kukejeli au kukemea mambo yanayoenda kinyume na maadili ya jamii
Uchambuzi wa Mashairi
1. Muundo/Umbo la Ushairi
Katika umbo wa shairi, tunaangazia jinsi shairi
lilivyoundwa kwa kuangazia mizani, vina, mishororo n.k Aidha, ni muhimu
kutaja aina na bahari za shairi zinazohusiana na kila sifa uliyoitaja.
2. Uhuru wa Mshairi
Mshairi hafungwi na kanuni za kisarufi za lugha
katika utunzi wa shairi. Anaweza kufanya makosa ya kisarufi kimakusudi ili
shairi lizingatie umbo fulani. Zifuatazo ni njia mbalimbali ambazo mtunzi wa
shairi anaweza kutumia kuonyesha uhuru wake.
3. Maudhui
Maudhui ni jumla ya ujumbe na mawazo mbalimbali
yanayojitokeza katika shairi fulani. Haya ni mambo yanayotajwa katika hadithi
na yanaweza kujumuisha mawazo zaidi ya moja. Maudhui husaidia kujenga dhamira
ya shairi.
4. Dhamira
Dhamira
ni lengo, dhumuni au nia ya mtunzi wa shairi. Mtunzi wa shairi anaweza kuwa
na kusudi la kutuonya, kututahadharisha au kutunasihi kuhusiana na jambo
fulani.
5. Mtindo wa Lugha
Mtindo wa lugha hurejelea namna mbalimbali
ambazo mshairi anatumia mbinu za lugha. Mshairi anaweza kutumia mbinu za
lugha. kama vile: Tanakali za Sauti, Istiara, Takriri, Semi n.k
|
0 التعليقات:
إرسال تعليق