الصفحة الرئيسية » » sambo ya kiwandeo

sambo ya kiwandeo



Sambo ya kiwandeo ni shairi kwa bahari ya utendi "utenzi"( shairi ndefu leny mishororo minne kila ubeti na mshororo haugawanywa na vipande.) ,mtungaji wake ni Ahmed Sheikh Nabahany na Ahmed Sheikh Nabahany ni moja wa washairi wakubwa katika Kiswahili na moja wa mwongozi wa mtendo wa urasimi mpya,alizaliwa tarehe 27 mwezi novemba mwaka 1927 BK wazazi wake walikufa wakati wa utoto wake na alilewa na nyanya wake Amina Abubakr Sheikh , na bibi huyu ni mshairi maarufu sana na moja kwa ushairi wake ni utendi wa "Ngamia na paa ", na Ahmed Sheikh Nabahany alirithi kipaji hicho kutoka nyanya wake na kutoka mashairi yake mashuri sana ni " Sifa za mnazi" yenye beti 79 na "Manukato ya wambedja" yenye beti 107,pamoja na Sambo ya kiwandeo.

Bahari ya utenzi wa sambo ya kiwandeo iliundwa kwa silabi /ya/. Utenzi huo una beti 217.utenzi una mishororo minne ,urari wa mizani katika kila mshororo ni mizani nane, mishororo mitatu ya kwanza ina kina kimoja ,na kina cha kituo (mshororo ya mwisho) ni kina cha bahari kilichokaririwa mwishoni mwa kituo katika kila ubeti hadi mwisho yaani ni bahari ya mtiririko. Utenzi ulitungwa kwa lahaja ya kiamu na kimvita .kiamu hasa kizingatiwa kama lahaja ya ushairi . Mshairi alitumia baadhi ya maneno kutokana lugha ya kiarabu lakini kwa matamshi ya kiswahili (Utohozi), pamoja na tamathali ya usemi na mbinu ya lugha kama sitiari,tashbiha, na hasahasa taswira,n.k
Anuani ya utendi ni sambo ya kiwandeo na kiwa ndeo ni kisiwa cha lamu na sambo ni jina la jahazi kubwa liliundwa zamani kale wakati wa mtume maarufu sana Nuhu (A.S). sambo iliandikwa na lahaja ya kiamu maudhui yake ni kueleza hali ya watu walioishi pwani hasa mjini lamu na ujuzi wao baharini hasa hasa kwenye kujenga jahazi na mtepe bela ya kutumia misumari lakini ubao ulifungwa na mwingine kwa kamba maalumu , sambo hii ni jahazi kubwa katika zama ya mtume Nuhu (A.S) , Baada ya kueleza namna ya kuundwa kwa jahazi na kusifu sehemu jahazini na namna ya kuitengeneza, Sheikh Nabahany  alieleza hali ya vipi jahazi kusafirishwa ili kuchukua bidhaa na waabiria kupita nchi mbalimbali kama Msumbiji , Bukini, Bara laArabu, na Bara la Hindi.
 Utenzi ulitungwa tarehe 18 mwezi aprili mwaka 1970 BK kama ilitajwa ubeti 214 ili kusajili na kuhifadhi sira ya jahazi hili kutoka mzizi hadi mwingine kama ilivyotajwa katika ubeti 208 hii ni dhamira ya utenzi.

0 التعليقات:

إرسال تعليق